Friday, July 27, 2012

UHOLANZI YASITISHA MSAADA KWA RWANDA

Serikali ya Uholanzi imesitisha msaada wa dola milioni 6.15 kwa Rwanda baada ya nchi hiyo kuhusishwa na udadhili wa waasi katika Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Hatua hii inajiri siku kadhaa baada ya Marekani kutangza inanuia kupunguza msaada wa kijeshi kwa Rwanda.

 
Hata hivyo Rwanda imekuwa ikikanusha madai ya umoja wa mataifa kuwa inafadhili kundi la waasi wa M23 mashariki mwa DR Congo. 
Waasi hao walianza kutoka jeshini kuanzia mwezi Aprili na hadi kufikia sasa takriban watu 200,000 wametoroka makwao kwa sababu ya mapigano kati ya jeshi na waasi hao.

Hatua hii ya Udachi inajiri baada ya afisaa mkuu wa umoja wa mataifa kuambia BBC kuwa wanajeshi wanaotoka katika jeshi la DRC wamekiri kusajiliwa na Rwanda.

Mnamo siku ya Alhamisi, Umoja wa mataifa uliripoti kuwa wanajeshi wake walisaidia jeshi la DRC kuwafukuza waasi hao kutoka mji wa Goma kwa kutumia helikopta pamoja na magari ya kijeshi.


Mfumo wa sheria

Mwandishi wa BBC mjii Hague, Anna Holigan, anasema kuwa hii ndio hatia ya kwanza ya kifedha kuwa rais Kagame huenda ameanza kuwapoteza washirika wake wa Ulaya.

Waziri wa mambo ya nje wa Uholanzi, amethibitisha kuwa kuanzia sasa haitafadhili vyovyote serikali ya Rwanda hadi pale itakapoweza kuhakikishiwa na Rwanda kuhusiana na madai hayo.

Pesa hizo ilizokuwa inapokea Rwanda zilikuwa zinatumika kuinia hadhi ya mfumo wa sheria wa Rwanda, ingawa mashirika yasiyo ya kiserikali yataendelea kufadhiliwa.

Serikali ya Udachi hata hivyo ingali inasubiri jibu kutoka kwa Rwanda kuhusiana na hatua hiyo wakati ikiendelea kushauriana na nchi zingine za Ulaya kuhusu hatua zaidi dhidi ya Rwanda.


BBC SWAHILI

No comments:

Post a Comment