Saturday, July 21, 2012

SUDAN KUSINI YASUSIA MAZUNGUMZO YA ANA KWA ANA

Sudan Kusini imevunja mazungumzo ya ana kwa ana na jirani yake, Sudan, yaliyopangwa kufanywa, baada ya kuishutumu Sudan kuwa imefanya mashambulio mengine ya ndege kwenye ardhi ya Sudan Kusini.
Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini

Msemaji wa ujumbe wa Sudan Kusini kwenye mazungumzo hayo mjini Addis Ababa, Atif Kiir, alisema kwamba mazungumzo hayo sasa yatafanywa kwa kupitia kamati ya Umoja wa Afrika.

Msemaji wa jeshi la Sudan, alieleza kuwa ndege za jeshi, zililenga wapiganaji waliovuka mpaka na kuingia Sudan.

Umoja wa Mataifa umezipa nchi hizo muda hadi tarehe mbili Agosti, kutatua ugomvi wao kuhusu mpaka na maswala ya usalama.

BBC SWAHILI

No comments:

Post a Comment