Saturday, July 28, 2012

MAZUNGUMZO YA SUDAN YAKWAMA TENA

Wapiganaji wa SPLM-North 
Wapiganaji wa Sudan wanasema kuwa mazungumzo na serikali ya Sudan kuhusu shida za watu karibu na mpaka wa Sudan Kusini, yamevunjika. 

Akizungumza na BBC, Yasir Arman wa chama cha SPLM North, ameishutumu serikali ya Sudan, kuwa inajaribu kuzusha maswala ya siasa kwenye mazungumzo, na wakati wake haukufika, alisema.

Bwana Arman alisema watu 1,000 wanavuka kila siku kutoka Blue Nile na Kordofan Kusini, na kuingia Sudan Kusini, ili kukimbia njaa na magonjwa - na hivo kuleta maswala ya siasa kwa sasa ni kutoa mazungumzo kwenye mkondo unaofaa.

Watu wengi wamekimbia mapigano, na hivo kuacha kilimo na kufanya watu wengi kukosa chakula. 
 

No comments:

Post a Comment