Saturday, July 21, 2012

DRC YAVITAKA VIKOSI VYA UMOJA WA MATAIFA VIENDELEE KUWEPO MASHARIKI MWA NCHI HIYO

Viongozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wamevitaka vikosi vya majeshi ya Umoja wa Mataifa kuendelea kuwepo mashariki mwa nchi hiyo kwa ajili ya kupambana na waasi wa M23.

Mjumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Congo hivi karibuni alitangaza kusikitishwa kwake na hali inayoendelea katika eneo la mashariki mwa nchi hiyo na kusema kuwa inatia wasiwasi. Wiki iliyopita pia msemaji wa vikosi vya UN nchini Congo alizungumzia hali ya eneo la mashariki mwa Congo na kusema kuwa, waasi wa Mai Mai wanadhibiti mji wa Walikale.

Duru za habari zinasema kuwa, kufuatia kushadidi kwa mapigano yanayofanywa na waasi hao mamia kadhaa ya askari wa Congo wamelazimika kukimbilia katika maeneo ya askari wa Umoja wa Mataifa kwa ajili ya kupata hifadhi. 

No comments:

Post a Comment