Thursday, July 26, 2012

RAIS KAGAME ATISHIWA KUSHITAKIWA ICC

Afisa mmoja wa ngazi ya juu nchini Marekani ameonya kuwa Rais wa Rwanda, Paul Kagame, huenda akafunguliwa mashtaka ya uhalifu wa kivita kwa kuhusika na vita katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Stephen Rapp, ambae ni mkuu wa kitengo cha jinai ya kimataifa nchini Marekani, amesema hii inatokana na madai kuwa Rwanda inawafadhili waasi wanaopigana katika mashariki mwa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo.
Afisa huyo amesema kuwa Rais Kagame huenda akashtakiwa katika mahakama ya jinai ya kimataifa katika The Hague kwa madai ya kuwafadhili waasi.

Ripoti ya hivi majuzi ya Umoja wa mataifa juu ya mzozo wa mashariki mwa Jamhuri ya Congo iliituhumu Rwanda kwa kuyawapa silaha makundi ya waasi.

Hata hivyo Rais Paul Kagame mwenyew amekanusha mara kadhaa kwamba serikali yake ina husika kivyovyote na hita hivyo vya Congo.

Kagame amepuuza habari hizi akisema kwamba maoni yao hayakujumuishwa na walioandika ripoti hizo za kuwalaumu.

No comments:

Post a Comment