Maafisa nchini afrika kusini
wanasema takriban watu 19 wameuwawa baada ya treni kugonga lori
lililokuwa limebeba wafanyikazi kwenye kivukio cha reli.
Ajali hiyo imetokea katika mkoa wa mashariki wa Mpumalanga.
Habari kamili kuhusu ajali hiyo bado hazijulikani kikamilifu.
Ingawa kuna taarifa nyengine ambazo zinasema kuwa watu wapatao 24 huenda wameuwawa.
No comments:
Post a Comment