Saturday, July 21, 2012

MBUNGE MISRI AKUTWA AKIFANYA MAPENZI NDANI YA GARI

Mbunge wa Misri wa chama cha Kiislamu chenye msimamo mkali, amepatikana na makosa ya kuvunja adabu ya kijamii, kuhusu tukio ambapo amekutwa anafanya mapenzi ndani ya gari lake.

Bunge la MIsri kabla ya kufungwa
Kesi hiyo imewatia aibu Waislamu wanaoitwa Salafi - ambao wanadai kuwa wanaume watengwe kabisa na wanawake.

Mbunge huyo, Ali Wanis, alipewa hukumu ya kifungo cha mwaka mmoja na nusu, kwa kufanya mapenzi na mwanafunzi, na kwa kumshambulia askari polisi.

Mbunge huyo ni wa chama cha Nour, kwenye bunge la mwanzo kuundwa baada ya utawala wa Rais Mubarak - bunge ambalo lilifutwa mwezi uliopita baada ya mahakama kuamua kuwa bunge hilo siyo halali.

No comments:

Post a Comment