Saturday, August 4, 2012

MAHARAMIA WASHAMBULIA MELI ZA MAFUTA NCHINI NIGERIA


Watu wenye silaha wameshambulia meli mbili nje ya eneo la mafuta la Nigeria, eneo la mdomo wa Mto Niger.
 
Walinzi wawili waliuwawa na wawili kujeruhiwa katika shambulizi hilo.

Washambuliaji hao, ambao hawakujulikana, pia waliwateka nyara mabaharia wanne.

Jeshi la wanamaji la Nigeria nalo linashiriki kuwasaka washambuliaji hao.

Shambulio hilo limetokea siku tu baada ya serikali ya Nigeria kutangaza kuwa itatumia satalaiti kuzuwia magendo ya mafuta katika eneo hilo, ambayo huuzwa kwenye soko la kimataifa. 
 

No comments:

Post a Comment